{"id":1570314,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1570314/?format=json","text_counter":205,"type":"speech","speaker_name":"Sen. (Dr.) Murango","speaker_title":"","speaker":null,"content":"Mstahiki Spika wa muda, katika falsafa yangu, nilisema ya kwamba katika siku mbaya, siku ya aibu ya kuku, upepo ambao unafungua kuku manyoya na kuiacha uchi huwa unatoka nyuma. Nilipeana mfano wa wale ambao watakuja nyuma na kuongea mambo mengi kwa sababu hawakuwa kwenye mkutano. Asante sana."}