{"id":1604091,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1604091/?format=json","text_counter":46,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Madzayo","speaker_title":"The Senate Minority Leader","speaker":null,"content":"Katika orodha yetu tuko na mambo mengine ambayo lazima tuyashughulikie. Lakini kwa sababu hili ni jambo la muhimu na la kitaifa na linahusika na kitengo cha polisi ambacho kimefanya kitendo kama hicho, ingekuwa bora zaidi kama Bunge hili la Seneti lingepewa nafasi kujadiliana sasa hivi ikiwa itawezekana. Naomba. Asante."}