{"id":1604154,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1604154/?format=json","text_counter":109,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Mwaruma","speaker_title":"","speaker":null,"content":"Nimehuzunika sana kwa kifo chake kwa sababu Bw. Albert Ojwang’ vile tumeambiwa alikuwa ni mtoto wa pekee katika familia yao. Pia, vile tumeona katika vyombo vya habari, ninajua kuwa babake alikuwa masikini. Alibebwa kutoka Homa Bay hadi kituo cha polisi hapa Nairobi kama kwamba hakuna vituo vya polisi kule Homa Bay."}