{"id":1604155,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1604155/?format=json","text_counter":110,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Mwaruma","speaker_title":"","speaker":null,"content":"Ni jambo la kuhuzunisha kwamba asasi za usalama zinatumika ili kuwanyamazisha Wakenya kwa sababu ya kuongea ukweli. Kama mambo hayaendi sawa, watu lazima wawe na uhuru wa kuongea. Tusirudishwe miaka ya zamani kwa sababu wakati huu tumeenda mbali sana."}