{"id":1604328,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1604328/?format=json","text_counter":283,"type":"speech","speaker_name":"Sen. (Dr.) Murango","speaker_title":"","speaker":null,"content":"Mchele mwingi tunaouenzi unatoka eneo la Mwea--- Umenikumbusha nikuletee angalau kilo mbili. Nitafanya hivyo, Bi. Spika. Maji ya kunywa Mwea yameadimika kama wali wa daku ama kaburi la baniani. Ukienda kule aidha uende kunywa mtoni au yaletwe kwa punda na ni maji machafu."}