{"id":1625081,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1625081/?format=json","text_counter":296,"type":"speech","speaker_name":"Sen. (Dr.) Murango","speaker_title":"","speaker":null,"content":"Asante sana, Bw. Naibu Spika. Kulingana na kanuni za Spika kwa mavazi, Seneta yeyote anafaa kuvalia vinavyotakikana. Sen. Tabitha Mutinda anatoa tafsida yake kwa mguu chuma. Hana viatu. Kwa kawaida, yeye huwa mrefu lakini saa hizi amekuwa mfupi kama mwezi wa Februari. Je, huo ni ungwana?"}