{"id":173343,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/173343/?format=json","text_counter":386,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Mwadeghu","speaker_title":"","speaker":{"id":98,"legal_name":"Thomas Ludindi Mwadeghu","slug":"thomas-mwadeghu"},"content":"Bw. Spika, jambo lingine ambalo ningependa kuchangia ni kuhusu bandari huru ambayo inatarajiwa kuwepo baadaye. Bandari hii isije ikavamiwa na makabaila au waporaji ambao wanangojea tu wakati Waziri atakapotangaza, wao watakuwa tayari kuwanyima wenzao haki zao. Ninamwomba Waziri ahakikishe kwamba Mswada huu umeangaliwa kikamilifu."}