{"id":173347,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/173347/?format=json","text_counter":390,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Mwadeghu","speaker_title":"","speaker":{"id":98,"legal_name":"Thomas Ludindi Mwadeghu","slug":"thomas-mwadeghu"},"content":"Tujiepushe na janga ambalo tumeliona kwa Wataliano kule Malindi ambapo hata vioski vya kawaida vimekuwa ni vyao. Mkenya akienda kutafuta kioski huko Italia ama Ulaya hatakipata. Lakini humu nchini tumeruhusu mtu yeyote kufanya atakavyo. Ninamwomba Waziri azingatie mambo haya na kuhakikisha kwamba Mswada huu umerekebishwa."}