{"id":208232,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/208232/?format=json","text_counter":220,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Rai","speaker_title":"","speaker":{"id":203,"legal_name":"Samuel Gonzi Rai","slug":"samuel-rai"},"content":"Mpaka itakapokuwa imepitishwa katika Bunge hili, na ianze kazi wakati itakapokuwa imepitishwa katika Bunge, ndipo nitakapotosheka kwamba pesa zile ni halali. Lakini, kwa sasa, ni haramu! Nai kiwa Bw. Ringera hawezi kufanya kazi kama hiyo, basi inaonekana pia na yeye ameshindwa. Atuambie na tuko tayari kumchagua mtu mwingine kufanya kazi hiyo. Kwa hayo machache ama mengi, napinga!"}