{"id":213866,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/213866/?format=json","text_counter":60,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Mwandawiro","speaker_title":"","speaker":{"id":253,"legal_name":"Mwandawiro JD Mghanga","slug":"mwandawiro-mghanga"},"content":"Jambo la nidhamu, Bw. Spika. Tangu jana tumekuwa tukipelekwa kizungumkuti na Wizara hii ikisema kuhusu sera au Mswada ambao utaletwa mbele ya Bunge hili. Swali langu lilikuwa halisi. Hivi sasa Wizara ina mipango gani ya kufidia wale watu ambao wamejeruhiwa au kuuawa hata kabla ya sisi kuijadili sera anayoizungumzia?"}