{"id":216844,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/216844/?format=json","text_counter":101,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Mwandawiro","speaker_title":"","speaker":{"id":253,"legal_name":"Mwandawiro JD Mghanga","slug":"mwandawiro-mghanga"},"content":"Bw. Spika, inaonekana wazi kwamba tunaimarisha utamaduni wa ufisadi. Ufisadi umetendeka na tunaonyesha Wakenya kwamba mtu anaweza kupasua ardhi ya umma na baadaye akigawa kidogo, tunamhurumia na kuacha ufisadi uliotendeka. Je, huu ni utamaduni wa kumaliza ufisadi? Je, Serikali inakubali kuendeleza utamaduni wa ufisadi?"}