{"id":220785,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/220785/?format=json","text_counter":41,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Mwandawiro","speaker_title":"","speaker":{"id":253,"legal_name":"Mwandawiro JD Mghanga","slug":"mwandawiro-mghanga"},"content":"Bw. Naibu Spika, hali ambayo tunaisikia kutoka kwa Serikali inasikitisha sana. Shule zinafungwa, watu wanalazimika kuhama makao yao na huku Waziri Msaidizi anasema kwamba wanahakikisha kwamba kuna usalama katika Mlima Elgon. Je, hii Serikali imeshindwa kuwahakikishia watu wa Mlima Elgon usalama au inakataa kuwapatia usalama?"}