{"id":222850,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/222850/?format=json","text_counter":125,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Mwandawiro","speaker_title":"","speaker":{"id":253,"legal_name":"Mwandawiro JD Mghanga","slug":"mwandawiro-mghanga"},"content":"Bw. Naibu Spika, mafuriko yanayokumba Mkoa wa Magharibi hasa sehemu za Budalang'i, Nyando na Nyanza Kusini hutokea mwaka nenda, mwaka rudi. Mafuriko hayo husababisha hasara kubwa, kwa mfano, huangamiza binadamu, mifugo na kuharibu mali. Je, ni mipango gani halisi ambayo Wizara inaweka ya kuondoa tatizo hili kabisa? Je, mipango hii itatimizwa lini?"}