{"id":226859,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/226859/?format=json","text_counter":30,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Mwandawiro","speaker_title":"","speaker":{"id":253,"legal_name":"Mwandawiro JD Mghanga","slug":"mwandawiro-mghanga"},"content":"Bw. Spika, Swali hili ni muhimu sana na si la kupuuzwa. Wakati makampuni yanajenga barabara huwa yanajenga kambi. Je, Wizara hii imechukua hatua gani ya kuyashawishi makampuni hayo kuzipatia jamii husika kambi hizo kutumia kama vyuo vya ufundi ama vituo vinginevyo? Wizara hii inafanya nini? Haitoshi kusema tu kwamba watu wayashawishi makampuni hayo."}