{"id":240544,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/240544/?format=json","text_counter":14,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Kingi","speaker_title":"","speaker":{"id":27,"legal_name":"Amason Jeffah Kingi","slug":"amason-kingi"},"content":"Bw. Naibu Spika, kazi ya machifu, manaibu wao na maofisa wengine wa utawala ni kushirikiana na wananchi ili usalama udumishwe. Wakati wowote maofisa hao wanapopeleka ripoti kwa maofisa wa polisi kwamba kuna vitendo vya uhalifu, hatua mwafaka huchukuliwa ili kuhakikisha vitendo hivi haviendelei."}