{"id":240921,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/240921/?format=json","text_counter":115,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Mwandawiro","speaker_title":"","speaker":{"id":253,"legal_name":"Mwandawiro JD Mghanga","slug":"mwandawiro-mghanga"},"content":"Bw. Spika, nimesikiliza jawabu la Waziri kwa makini sana. Ametoa orodha ya hatua ambazo zimechukuliwa kulinda Jiji la Nairobi ili lisipatwe na majanga. Ukweli ni kwamba, mitaa ya mabanda yamejaa hapa jijini. Hakuna mpango kabisa! Je, Waziri anaweza kutueleza ni lini Wizara itachukua hatua na kutekeleza sheria za jiji ili kuhakikisha kwamba jiji hili litakabiliana na majanga na kuhakikisha kwamba halitakuwa mtaa mkubwa wa mabanda katika Afrika?"}