{"id":241259,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/241259/?format=json","text_counter":105,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Mwandawiro","speaker_title":"","speaker":{"id":253,"legal_name":"Mwandawiro JD Mghanga","slug":"mwandawiro-mghanga"},"content":"Bw. Spika, inasikitisha sana kuwa hadi sasa Wizara ya Leba inaendelea kuwepo wakati wafanyakazi wanaendelea kupata taabu kila mara kwa kisingizio kwamba kampuni imefilisika, mambo yako kortini na kadhalika. Bw. Spika, je, ni mikakati gani Wizara ya Leba imepanga kuhakikisha wafanyakazi hawataendelea kunyanyaswa nchini kwa sababu ya kisingizio kimoja ama kingine milele?"}