{"id":247632,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/247632/?format=json","text_counter":28,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Mwandawiro","speaker_title":"","speaker":{"id":253,"legal_name":"Mwandawiro JD Mghanga","slug":"mwandawiro-mghanga"},"content":"Bw. Naibu Spika, Waziri Msaidizi hajalihakikishia Bunge hili kwamba hakuna mfanyakazi atakayeachishwa kazi kwa sababu ya utumiaji wa mashine hizo. Yeye amesema tu kwamba kampuni hizo hazitawaachisha watu kazi. Je, Serikali itahakikisha vipi kwamba hakuna mfanyakazi atakayeachishwa kazi kutokana na kuletwa kwa mashine hizo?"}