{"id":247908,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/247908/?format=json","text_counter":91,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Mwandawiro","speaker_title":"","speaker":{"id":253,"legal_name":"Mwandawiro JD Mghanga","slug":"mwandawiro-mghanga"},"content":"Bw. Naibu Spika, ikichukuliwa kwamba maofisa wa Wizara ya Maji na Unyunyizaji Maji Mashambani, wahandisi na hata masorovea wanadai pesa nyingi sana wakati wanatoa huduma kwa pesa za maeneo Bunge, je, Waziri, maofisa wako wanafaa kulipwa shillingi ngapi ikiwa wanafikiri kwamba pesa za maeneo Bunge si mradi wa Serikali? Kuna taratibu gani ya kuwalipa maofisa hao wakati wanafanya miradi ya pesa za maeneo Bunge?"}