{"id":249952,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/249952/?format=json","text_counter":127,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Gitau","speaker_title":"","speaker":{"id":162,"legal_name":"William Kabogo Gitau","slug":"william-kabogo"},"content":"Bw. Naibu Spika, Waziri Msaidizi amesema kuwa hakuna magari ya kuzima moto kwa sababu Serikali ni lazima ifuate taratibu za ununuzi. Tunajua kuwa kashfa ya Anglo Leasing ilifanyika hapa nchini. Kwa nini hawakufuata taratibu hizo wakati huo?"}