{"id":251579,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/251579/?format=json","text_counter":127,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Mwandawiro","speaker_title":"","speaker":{"id":253,"legal_name":"Mwandawiro JD Mghanga","slug":"mwandawiro-mghanga"},"content":"Bw. Naibu Spika, ni jukumu la Serikali, hasa Mawaziri, kuhakikisha kwamba kuna umoja wa kitaifa kila pahali. Vile inavyoonekana, umoja wa kitaifa haukuzingatiwa na Wizara ya Afya. Walizingatia maslahi yao ya kibinafsi. Ni makosa sana kufanya hivyo. Je, Wizara ya Afya ina mipango gani ya kuhakikisha kwamba hakuna ukabila wakati inaajiri watu na kwamba, inazingatia umoja wa kitaifa?"}