{"id":251817,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/251817/?format=json","text_counter":51,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Mwandawiro","speaker_title":"","speaker":{"id":253,"legal_name":"Mwandawiro JD Mghanga","slug":"mwandawiro-mghanga"},"content":"Bw. Spika, Swali hili ni muhimu sana, na ni lazima lipewe uzito unaostahili. Hivi ninavyozungumza, kuna watu zaidi ya 30 katika mtaa wa Dandora ambao wamekufa mikononi mwa polisi. Je, Serikali inafanya nini kurekebisha hali hii ambapo wananchi wanazidi kupoteza maisha yao mikononi mwa polisi, akizingatia matukio ya mtaa wa Dandora?"}