{"id":252291,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/252291/?format=json","text_counter":84,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Mwandawiro","speaker_title":"","speaker":{"id":253,"legal_name":"Mwandawiro JD Mghanga","slug":"mwandawiro-mghanga"},"content":"Ahsante sana, Bw. Spika. Uvamizi wa wadudu waharibifu pia umetokea katika sehemu za Wundanyi na nyanda za chini za Wilaya ya Taita-Taveta kwa jumla, na kusababisha upungufu mkubwa sana, na haswa wa mbegu. Je, Waziri Msaidizi anaweza kueleza ni lini mbegu alizoahidi zitatolewa kwa wakulima? Je, ni lini atawapelekea wakulima mbegu hizo? Mvua inaendelea kunyesha na mbegu bado zinahitajika."}