{"id":258215,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/258215/?format=json","text_counter":490,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Kabogo","speaker_title":"","speaker":{"id":162,"legal_name":"William Kabogo Gitau","slug":"william-kabogo"},"content":"Hoja ya Nidhamu, Bw. Spika. Umemsikia Dr. Shaban akifafanua kuwa biashara zinazofanywa ni kama wale waliotajwa hata na Waziri kuhusu mambo ya madawa ya kulevya. Mimi nilitajwa, lakini baadaye Waziri alikuja akasema kwamba hakupata lolote wala chochote. Hakuna chochote kilitajwa hapa kunihusisha na madawa ya kulevya. Kisha, akaepa na maneno hayo akitumia Kiswahili cha kufurahisha. Kama ni sawa, akayaseme nje."}