{"id":301519,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/301519/?format=json","text_counter":211,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Ethuro","speaker_title":"","speaker":{"id":158,"legal_name":"Ekwee David Ethuro","slug":"ekwee-ethuro"},"content":"Hoja ya nidhamu, Bwana Naibu Spika. Ningependa kukashifu Waziri wa Kawi ambaye ana wasaidizi wawili, kwa hivyo wote ni watatu. Waziri wa Kawi amekawia kupeleka umeme eneo la Bura ambalo halijapata umeme tangu tupate Uhuru. Pia, Waziri huyu amekawia kuja Bunge. Ni vyema Waziri ambaye anapaswa kupeleka umeme katika sehemu ambayo haijakuwa na umeme tangu Uhuru bado anaendelea kukawia? Utafanya nini ili kuhakikisha kwamba Waziri huyu hakawii tena?"}