{"id":302764,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/302764/?format=json","text_counter":102,"type":"speech","speaker_name":"Ms. Leshoomo","speaker_title":"","speaker":{"id":379,"legal_name":"Maison Leshoomo","slug":"maison-leshoomo"},"content":"Bwana Spika, ningependa kumuuliza Waziri kuhusu mambo ya vitambulisho. Nimetoka Samburu leo na nilikuwa huko kwa siku nne. Wasamburu ambao hawana vitambulisho ni 8,000. Hawa watu watakuwa 8,000 vipi na kila siku katika magazeti, tunasoma kwamba Waziri ameshapeana vitambulisho? Pia, kwa nini watu wengine ambao wamewasilisha maombi ya vitambulisho wamekaa miaka miwili sasa na cheti cha kungoja?"}