{"id":315881,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/315881/?format=json","text_counter":153,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Mwadeghu","speaker_title":"","speaker":{"id":98,"legal_name":"Thomas Ludindi Mwadeghu","slug":"thomas-mwadeghu"},"content":"Asante, Bw. Spika. Ninaomba Waziri atufafanulie ni mikakati gani walionayo kuhusu hawa vijana wa boda boda na ajali ambazo zinatokea kila wakati. Ukienda katika hospitali nyingi, utakuta chumba maalum kimewekwa kuwaangalia majeruhi wa boda boda. Wizara inaangalia jambo hili bila kuchukua hatua yoyote."}