{"id":329797,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/329797/?format=json","text_counter":1053,"type":"other","speaker_name":"","speaker_title":"","speaker":null,"content":"Mwisho ni kwamba Bunge hili limefanya kazi, lakini tunapoenda nyumbani, ni kama tunaonekana bado tunahitajika kufanya kazi zaidi. Naomba wananchi waelewe kwamba Bunge hili limefanya kazi kubwa. Tumechangia Miswada mingi. Tulipitisha Katiba mpya na kufanya mambo mengi mazuri. Kama binadamu hawatatambua kwamba tumefanya hayo yote, Mungu atatambua na kutuwezesha kwenda mbele. Kwa hayo mengi, ninaiunga Hoja hii mkono."}