{"id":352584,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/352584/?format=json","text_counter":144,"type":"other","speaker_name":"","speaker_title":"","speaker":null,"content":"na akina mama wanalala watatu kitanda kimoja pamoja na watoto wao. Hakuna madawa. Hakuna vifaa bora vinavyohitajika. Kina mama wanapokwenda kwa upasuaji wanapanga laini. Wengine wanakufa njiani wakiwa hawajafikia matibabu. Tungetaka kujua mikakati mwafaka ambayo itaweza kuhakikisha akina mama hawatalipa kitu, na watapata huduma bora. Hatutaki bora huduma; tunataka huduma bora. Elimu ya bure imekuwa bora elimu lakini si elimu bora. Tunataka huduma bora."}