{"id":360608,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/360608/?format=json","text_counter":344,"type":"speech","speaker_name":"Hon. S.A. Ali","speaker_title":"","speaker":{"id":2100,"legal_name":"Shariff Athman Ali","slug":"shariff-athman-ali"},"content":"Ahsante Mhe. Spika wa Muda. Kwanza, ninataka kumshukuru ndugu yangu, Mheshimiwa aliyeleta Hoja hii hapa. Tunafahamu vyema kwamba wazee wetu ni watu ambao wanahitaji kuzingatiwa sana. Hii ni kwa sababu hatungefika hapa leo au hatungefikisha umri huu bila wazee wetu. Hata sisi tutakuwa wazee."}