{"id":363515,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/363515/?format=json","text_counter":105,"type":"speech","speaker_name":"Hon. Wario","speaker_title":"","speaker":{"id":252,"legal_name":"Ali Wario","slug":"ali-wario"},"content":"Katika ukurasa wa saba wa hii Ripoti, utaona kwamba Kamati inasema wateuliwa hawa hawana visa vya ufisadi na wamelipa kodi. Wamesafishwa. Ni kwa nini wasipewe zawadi? Kama wewe huhusiki na ufisadi, na unalipa kodi kila siku, unastahili kupewa bendera uende nayo nyumbani."}