{"id":363524,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/363524/?format=json","text_counter":114,"type":"other","speaker_name":"","speaker_title":"","speaker":null,"content":"Nikimalizia mchango wangu, kuna akina dada wanaotolewa Kenya na kupelekwa Saudi Arabia na sehemu nyingine ulimwenguni kufanya kazi. Akina dada hao wanadhulumiwa na kunyanyaswa. Kwa hivyo, ninamwomba mhe. Kambi ayaangazie masuala ya ajira, na hasa suala la wale akina dada wanaokwenda kutafuta kazi kule Saudi Arabia."}