{"id":371137,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/371137/?format=json","text_counter":202,"type":"speech","speaker_name":"Hon. (Ms.) Chidzuga)","speaker_title":"","speaker":{"id":751,"legal_name":"Zainab Kalekye Chidzuga","slug":"zainab-kalekye-chidzuga"},"content":"Kenya imekuwa na uzoefu wa watu kuzungumzia ufisadi lakini hakuna hatua inayochukuliwa. Tume nyingi sana zimeundwa kwa kisingizio kwamba zitachunguza ufisadi na kuleta ripoti. Mwishowe, zile ripoti zinawekwa kwa makabati na Mkenya anaendelea kuwa maskini. Ndio mpaka leo tunashindwa kuwalipa walimu wetu. Pesa ziko lakini hatutaki kutenda haki. Naunga mkono Hoja hii ili tuisafishe nchi yetu, tuaminike hata katika ulimwengu wote kwamba Kenya iko tayari kuisafisha nyumba yake na tuweze kutimiza haki kwa watu wetu."}