{"id":373784,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/373784/?format=json","text_counter":240,"type":"speech","speaker_name":"Hon. Dukicha","speaker_title":"","speaker":{"id":1480,"legal_name":"Hassan Abdi Dukicha","slug":"hassan-abdi-dukicha"},"content":"KenGen na TARDA zimekuwa ni mzigo kwa watu wa Tana River na Kenya kwa jumla. Nasema hivyo kwa sababu tangu KenGen na TARDA zianze kujenga mabwawa, wamefuga mamba wengi sana. Kila wakati, watu wetu wanachukuliwa na mamba kando kando ya mto."}