{"id":373785,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/373785/?format=json","text_counter":241,"type":"speech","speaker_name":"Hon. Dukicha","speaker_title":"","speaker":{"id":1480,"legal_name":"Hassan Abdi Dukicha","slug":"hassan-abdi-dukicha"},"content":"Vile vile, mafuriko ambayo TARDA inasababisha yameathiri pakubwa au kuharibu mimea kama vile ndizi na maembe. Sisi katika Tana River tunajivunia maembe. Katika Kenya nzima, sisi ndio tunaongoza katika uzalizaji wa maembe. Vile vile, tunapanda ndizi. Lakini hatupati faida kwa sababu ya mafuriko ambayo yanasababishwa kila wakati na KenGen."}