{"id":378323,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/378323/?format=json","text_counter":416,"type":"other","speaker_name":"","speaker_title":"","speaker":null,"content":"Jambo la pili, ukituangalia vile tuko hivi, tuna wafanyikazi ambao Serikali inatakiwa iwalipe ndio watufanyie kazi na hawajalipwa. Tunatakiwa tuwe na afisi ambazo Serikali inatakiwa kulipia lakini hazijalipiwa. Ingekuwa vizuri hili jambo tulimalizie hapa, tukubaliane kama tunapitisha Mswada wa VAT na vile pesa zetu tutapewa kabla hatujaondoka."}