{"id":390781,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/390781/?format=json","text_counter":263,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Bule","speaker_title":"","speaker":{"id":1029,"legal_name":"Ali Abdi Bule","slug":"ali-abdi-bule"},"content":"Kwa Hoja ya nidhamu, Bw. Naibu Spika. Kwa kweli mazungumzo mengine huwa yanaleta utata na uchochezi mahali kama hapa. Wakati huu Wakenya tunaungana na kutafuta mahali ambapo kuna ubaya. Tunataka kusuluhisha mabaya lakini hatutaki kuleta makuu hapa Kenya. Ikiwa Seneta anataja sehemu fulani ama jamii fulani, ataleta utata na uchokozi. Kwa hivyo, anataka kuleta vurugu hapa Kenya na hiyo sio sawa. Kwa hivyo ni lazima aombe msamaha---"}