{"id":413001,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/413001/?format=json","text_counter":753,"type":"other","speaker_name":"","speaker_title":"","speaker":null,"content":"Jambo lingine ambalo linafanya nipinge Mswada huu ni kuhusu ile Tume ya Mishahara na Marupurupu. Utakuta Makamishina wengine pamoja na Mwenyekiti wanatakikana kufanya kazi mfurulizo na wengine waje kwa muda. Hilo si jambo nzuri. Ikiwa tutapitisha Mswada huu, basi watapatiwa muhula mwingine wa miaka sita. Hivyoni kinyuma na Katiba yetu."}