{"id":425430,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/425430/?format=json","text_counter":273,"type":"speech","speaker_name":"Sen. (Dr.) Machage","speaker_title":"","speaker":{"id":179,"legal_name":"Wilfred Gisuka Machage","slug":"wilfred-machage"},"content":"Huu ni ukweli kwa sababu hatutaki kuyasema hapa kwa sababu leo tunaongea mambo ya Kaunti ya Embu. Lakini yaliyoko huko ni mazito hata kuliko ya Embu kwa sababu walikataa kuskia la mkuu. Sisi Maseneta tukiwambia hawasiki, wakatudharua, hawataki kusikia wasia wetu, basi majuto ni mjuku. Walijitosa kwa ulimwengu wa anasa, magari makubwa makubwa, ma askari wawafuatilia na magari mengi na bendera ya kupepea, wakasahau ya kwamba mbio za sakafuni huishia ukingoni. Sasa wamejua mkubwa ni nani."}