{"id":442410,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/442410/?format=json","text_counter":326,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Madzayo","speaker_title":"","speaker":{"id":679,"legal_name":"Stewart Mwachiru Shadrack Madzayo","slug":"stewart-mwachiru-shadrack-madzayo"},"content":"Hoja ya nidhamu, Bw. Naibu Spika. Je, ni haki kwa Sen. Elachi, akiwa Kiranja wa Wengi katika Seneti, kutaja kabila fulani? Seneti hii yaongea kuhusu Wakenya waliokufa na si watu wa kabila fulani. Ikiwa mambo yataenda hivyo, kati ya waliokufa huko Lamu pia kuna Waislamu na Wakristu."}