{"id":473665,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/473665/?format=json","text_counter":224,"type":"speech","speaker_name":"Hon. (Ms.) Khamisi","speaker_title":"","speaker":{"id":874,"legal_name":"Mishi Juma Khamisi","slug":"mishi-juma-khamisi"},"content":"Pia, Sura ya Nne, Aya 13 inazungumzia wale ambao ni walemavu katika kupata haki zao. Inasema kuwa miundomisingi lazima iwawezeshe walemavu ambao wameathiriwa kupata haki yao. Tunaona katika mahakama zetu mwathiriwa ambaye ni mlemavu anashindwa kufika katika kizimbani ama kuingia katika mahakama na hii ni kwasababu ya vile imejengwa, miundo misingi yake haikuzingatiwa."}