{"id":473668,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/473668/?format=json","text_counter":227,"type":"speech","speaker_name":"Hon. (Ms.) Khamisi","speaker_title":"","speaker":{"id":874,"legal_name":"Mishi Juma Khamisi","slug":"mishi-juma-khamisi"},"content":"Tumeona wengi wameuwawa kwa njia hii. Kwa lugha ya Kiingereza tunasema “ mob justice ”. Unaweza kuwa na chuki na mtu fulani, unapiga nduru na kusema huyu mtu ni mwizi ama huyu mtu amefanya jambo fulani. Huyo mtu anauwawa na tunakosa haki kwa watu kama hao."}