{"id":526192,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/526192/?format=json","text_counter":24,"type":"other","speaker_name":"","speaker_title":"","speaker":null,"content":"walivyosema ni kana kwamba wanajua. Basi kama wao ni Wakenya wazalendo, wamtaje. Vyombo vya usalama vipewe nafasi lakini wasizembee kwa kazi yao ya kumtafuta muuaji huyu; waachwe wafanye kazi yao. Lakini la kuumiza moyo ni kwamba inabainika labda kwamba nchini kuna vikundi ambavyo vimejitenga na kujiandaa kwa minajili ya kununuliwa kuua watu ilhali tunaambiwa kuwa kuna usalama, uchunguzi na makachero. Hao wamelala kazini! Hivyo ni vikundi vya kutafutwa na kutambuliwa."}