{"id":541219,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/541219/?format=json","text_counter":37,"type":"speech","speaker_name":"Hon. (Ms.) Chidzuga","speaker_title":"","speaker":{"id":751,"legal_name":"Zainab Kalekye Chidzuga","slug":"zainab-kalekye-chidzuga"},"content":"Tunaomba tuendeleze vita dhidi ya ufisadi. Kama vile Rais wetu alivyojitolea, na sisi pia tujitolee hivyo hivyo ili tuweze kusafisha hali hii ambayo imetuharibia uchumi wetu. Barabara zetu zinahitaji pesa nyingi sana ili zirekebishwe na kuwekwa katika hali ambayo inastahili. Hatuwezi kufikia kiwango hicho ikiwa ufisadi unaotendeka katika vituo vyetu vya kupima mizani hautakabiliwa vilivyo."}