{"id":563078,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/563078/?format=json","text_counter":84,"type":"speech","speaker_name":"Hon. (Ms.) Chidzuga","speaker_title":"","speaker":{"id":751,"legal_name":"Zainab Kalekye Chidzuga","slug":"zainab-kalekye-chidzuga"},"content":"Vilevile, ningependa kuiomba hii Kamati iweze kuangalia kiundani wakati hii ardhi inagawanywa, waweze kujua kama akina mama nao wamepata vipande vya ardhi kwa sababu sisi katika mila za Kiafrika, utakuta akina mama hawana kipande cha ardhi ambacho kinahesabika kwa jina la mama. Kwa hivyo, hii Kamati iangalie wakati ardhi inagawanywa, akina mama pia wapate sehemu za ardhi nao waweze kujivunia kama vile Wakenya wengine wanvyojivunia."}