{"id":642021,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/642021/?format=json","text_counter":113,"type":"speech","speaker_name":"Hon. Mwanyoha","speaker_title":"","speaker":{"id":2308,"legal_name":"Hassan Mohamed Mwanyoha","slug":"hassan-mohamed-mwanyoha"},"content":"tulipokuwa kule Malindi ambako tulilibeba kombe, nilifuatwa na vijana zaidi ya 2,000 ambao walikuwa wanajua kwamba mimi ni rafiki wa Mwenyekiti wa KADU Asili. Walijua kwamba nilikuwa nikimfanyia kampeini mwenyekiti huyo. Vijana hao walikuja mbio na kadi ambazo hazikuwa za vitambulisho vya kawaida. Wakanilalamikia kwamba wao wanataka wapige kura. Ukweli ni kwamba kama nilikuwa Jilore peke yake na nilipata vijana 2,000 wa KADU Asili---"}