{"id":642043,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/642043/?format=json","text_counter":135,"type":"speech","speaker_name":"Hon. Mwanyoha","speaker_title":"","speaker":{"id":2308,"legal_name":"Hassan Mohamed Mwanyoha","slug":"hassan-mohamed-mwanyoha"},"content":"Ninakushukuru sana kwa kuelewa yale maneno ambayo nilikuwa ninayazungumza. Ninaomba kila Mkenya aweze kupata nafasi nzuri anapofikisha umri wa miaka 18, ili apewe nafasi ya kuchukua ile stakabadhi ya kwanza na hiyo iwe inatumika. Sioni haja ya watu kuomba stakabadhi na kusubiri kwa miezi mitatu au minne. Maombi yote ya stakabadhi hiyo yanafaa kushughulikiwa mara moja ili mtu aweze kupata kitambulisho siku ya pili. Ahsante, Mhe. Naibu Spika wa Muda."}