{"id":648201,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/648201/?format=json","text_counter":386,"type":"speech","speaker_name":"Hon. (Ms.) Katana","speaker_title":"","speaker":{"id":691,"legal_name":"Aisha Jumwa Katana","slug":"aisha-jumwa-katana"},"content":"Kina mama ama jinsia ya kike katika taifa hili na katika ulimwengu mzima si kitu ambacho kinaweza kuangaliwa na jicho moja likiwa limefungwa. Tumeona nchi ambazo zimestawi na zile zimeendela, na Kenya ni moja kati ya zile ziliorodheshwa, zimepata kupiga hatua lakini tunajivuta nyuma kwa sababu ya kukosa uakilishi wa jinsia ya kike."}