{"id":685093,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/685093/?format=json","text_counter":1186,"type":"speech","speaker_name":"Hon. (Ms.) Korere","speaker_title":"","speaker":{"id":13134,"legal_name":"Sara Paulata Korere","slug":"sara-paulata-korere"},"content":"Nashukuru, Naibu Spika. Ni kitu cha maana kwamba katika Mswada huu, tumeeleza jinsi ujenzi wa barabara utakavyotekelezwa. Imekuwa taabu kubwa sana hasa kuhusu jinsi ambavyo serikali za kaunti zinajenga barabara. Kwa hivyo, nataka kupongeza Kamati iliyowasilisha Mswada huu. Ni matumaini yetu makubwa kwamba mahali kulikosahaulika kutakuwa na mabadiliko hivi karibuni. Nashukuru."}