{"id":757495,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/757495/?format=json","text_counter":49,"type":"speech","speaker_name":"Hon. Ali Wario","speaker_title":"","speaker":{"id":252,"legal_name":"Ali Wario","slug":"ali-wario"},"content":"Ahsante sana Mhe. Spika kwa kunipatia fursa hii. Kwanza kabisa, nasimama kuunga mkono Hoja ambayo imeletwa na Kiongozi wa Walio Wengi. Kifungu cha kwanza cha Katiba ya Kenya kinasema mamlaka ni ya mwananchi. Anaweza kuyatumia moja kwa moja ama kupitia kwa viongozi waliochaguliwa. Kifungu 95(2) cha Katiba ya Kenya kinasema Bunge itajadili chochote kinachomwathiri mwananchi wa Kenya."}